Na Veronica Mrema
Kisa
cha mwanamke mwenye umri mdogo ambaye aligundulika na saratani ya matiti, u kwenye matibabu
ya ki-bingwa kwa mwaka mmoja sasa, kinagusa mioyo ya wengi.
Ndani
ya ukumbi mdogo ulipo kwenye makazi ya Balozi wa Sweden nchini Tanzania, macho yangu yanashuhudia Balozi Charlotta
Ozaki Macias akichukua ‘tishu’ mezani kwake na kufuta machozi.
Tupo
zaidi ya wanawake 20 ndani ya ukumbi huu, tumefika kwa mwaliko wa Balozi
Charlotta ikiwa ni mwezi mahususi wa uelimishaji jamii kuhusu saratani hiyo, ‘Pink
October’.
Balozi
Charlotta ndiye mgeni rasmi anayezindua semina hii ya siku moja, aliyoalika pia
Shujaa Cancer Foundation ili kuwaelimisha wafanyakazi wa ubalozi, kuna
waliotoka balozi nyingine kadhaa pia.
Kila
meza aliipatia ‘assignment’ “Naomba kabla sijazindua, msalimiane, mjadiliane
kidogo kwa nini mmekuja hapa na unatarajia kujifunza nini?.
Hapo
ndipo ilipotoka simulizi fupi ya kisa cha Emilly Bavu, mwanamke mdogo
anayepambana na saratani ya matiti.
Emily
alijenga desturi ya kuchunguza matiti yake kufuatia kifo cha mama yake mzazi
aliyekutwa na ugonjwa huo pia.
Miezi
kadhaa kupita tangu kifo cha mama yake alibaini tofauti ndogo katika titi lake
la kushoto.
Baadae iligundulika naye ana saratani ya matiti na kuanza matibabu ni miaka miwili sasa akipatibiwa [makala haya tutakueletea kwa ukubwa na undani wake, siku zijazo].
Simulizi
ya leo ni ya Balozi Charlotta, mahojiano maalum na M24 TANZANIA MEDIA, karibu ufuatane nasi...
“Unajua
kwanini nimelia, naelewa anachokipitia. Mimi pia niliugua saratani ya matiti, nikiwa
Sweden .., ni safari ngumu,” anasema.
Anaongeza
“Miaka 10 iliyopita, nikiwa na umri wa miaka 4 na mama wa wasichana warembo wawili
[wadogo], nilipogundulika nina saratani ya matiti.
Ni
jambo lililomshtua kwa sababu mtindo wake wa maisha ulikuwa mzuri namna ile
inavyoshauriwa na wataalamu wa masuala ya afya, alijiweka mbali na vihatarishi
vinavyoweza kusababisha saratani.
“[Ukweli] sikuamini kama mimi ningepata saratani ya matiti. Nilidhani labda [anastahili kuugua] mtu mwingine, lakini si mimi,” anasimulia kwa utulivu.
NINI KILITOKEA?
Alianza
kuhisi maumivu katika matiti yangu na mikononi, alidhani labda ni kwa vile alitumia
muda mwingi kufanya kazi kwa ‘kompyuta’ yake.
Anasimulia
zaidi, “Niliamua kwenda kuonana na mtaalamu wa mazoezi tiba (physiotherapist). Lakini
mtaalamu huyo alinituma kwa daktari kwa
uchunguzi zaidi.
“Baada
ya kufanyiwa [uchunguzi kwa kipimo cha] mammografia, matokeo yalionesha nilikuwa
na uvimbe mkubwa wa sentimita 5.5.
“Hapo
ikawa mwanzo wa safari yangu ngumu, ya matibabu dhidi ya saratani,” anasimulia Balozi
Charlotta na kuongeza,
“[Yaani]
ghafla [maisha yalibadilika], nilijikuta nikianza safari iliyodumu takribani
mwaka mmoja, nikiwa kwenye tiba ya kemikali (chemotherapy), upasuaji na mionzi
(radiotherapy)”.
Anasema
safari hiyo haikuwa rahisi, kwani alipitia changamoto nyingi ikiwamo kushuka
kwa kinga mwilini, maambukizi ya mara kwa mara na uchovu mkubwa.
“Wakati
huo huo, nilikuwa na jukumu la kulea watoto wangu wadogo, lakini nilikuwa na
bahati.
“..,
kwa sababu nchini Sweden tuna mfumo mzuri wa afya unaofadhiliwa na Serikali.
Sikulazimika kulipa gharama za matibabu.
“Pia
nilipatiwa likizo ya ugonjwa bila kupoteza mshahara wangu wote. Kwa hiyo
nililindwa ki-fedha [uchumi] na nikaweza kuzingatia matibabu,” anasema.
UCHUNGUZI MAPEMA
Somo
kubwa la kujifunza katika visa vyote viwili [cha Emilly na Balozi Charlotta] ni
kwamba elimu kuhusu saratani ni muhimu kumfikia kila mmoja.
Uchunguzi
wa mapema pia ni jambo la msingi kulizingatia, Balozi Charlotta anasisitiza “Nimeeleza
kwamba sikuwahi kufikiria kama ningekuwa miongoni mwa waliougua saratani.
“[Kwa
sababu] nilikuwa mlaji mzuri wa mbogamboga kwa miaka mingi, nafanya yoga na
michezo mingine pia, sivuti sigara na pombe nilikuwa nakunywa kiasi kidogo mno.
“Pia
sina historia ya mtu aliyewahi kuugua saratani yoyote ile katika familia ya
baba na mama yangu, kwa hiyo nilidhani niko salama.
“Lakini, nilipougua nilijifunza somo muhimu; saratani inaweza kumtokea mtu yeyote, hata yule mwenye mtindo bora wa maisha na asiye na historia ya ugonjwa huu kwenye familia yake,” anasema.
SHAHIDI ZA KI-SAYANSI
Ni
hoja inayoungwa mkono pia na shahidi nyingi za ki-sayansi zilizofanyika kwa
miaka mingi hadi sasa duniani.
Asilimia
90 ya watu wanaougua magonjwa ya saratani ikiwamo hiyo ya matiti hawakuwahi
kuwa na historia ya ugonjwa huo ndani ya familia zao.
Ni
10% tu ya wagonjwa wote duniani ambao wana historia ya kuwahi kupata mgonjwa wa
saratani katika familia zao.
Daktari
Bingwa wa Magonjwa ya Saratani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Shaban Juma
anasema pamoja na hayo, kuna vihatarishi vinavyoweza kuchangia mtu kupata
magonjwa ya saratani.
“Kuna sababu zisizoweza
kubadilika ikiwamo za urithi wa vinasaba, kupata hedhi katika umri mdogo,
kuchelewa kukoma hedhi, kuwa na msongamano mkubwa wa ‘tishu’ katika matiti,
“Kuna sababu zinazoweza kubadilishwa kama vile uzito kupita kiasi,
unywaji wa pombe, ukosefu wa mazoezi, na matumizi ya homoni baada ya kukoma
hedhi.
Anaongeza “Shirika la Afya Duniani (WHO) sasa linabainisha wazi kuwa hakuna
kiwango salama cha unywaji pombe, likisisitiza umuhimu wa kuzingatia mtindo
bora wa maisha.
Kwa upande mwingine, wataalamu wanasema kuwa kuwa na watoto na kunyonyesha
mara kwa mara hupunguza hatari ya kupata saratani ya matiti.
Kwa sababu kipindi cha kunyonyesha humpa mwili mapumziko kutokana na homoni
ambazo zinahusiana na mzunguko wa hedhi.
Hata hivyo, kuchelewa kupata mtoto zaidi ya umri wa miaka 30 huongeza hatari. Licha ya saratani hii kuhusishwa zaidi na wanawake, wanaume nao huugua, ingawa ni kwa 1%.
MATIBABU HUTOFAUTIANA
Si
kila mgonjwa hupewa matibabu ya aina moja, hutofautiana kati ya mmoja na
mwingine.
Dkt.
Juma anafafanua zaidi, “Matibabu hutegemea aina ya saratani [aliyonayo mgonjwa
husika] na yanaweza kujumuisha upasuaji, chemotherapy, tiba ya homoni au tiba
ya mionzi.
Anasema
Tanzania kama ilivyo kwa mataifa mengine yanayoendelea, inazidi kuchukua hatua
katika kupambana na magonjwa ya saratani.
“Kwa
kupitia elimu kwa umma, kuimarisha huduma za afya ngazi ya msingi ili kusogeza
uchunguzi wa mapema karibu zaidi na jamii, upatikanaji wa huduma bora matibabu
pia,” anasema.
Anaongeza
“Lakini ni muhimu kujua pia uhai wa mgonjwa hauishii baada ya matibabu, wengine
hukumbwa na changamoto za kimwili, kisaikolojia, na kijamii.
“Hivyo,
msaada wa familia na jamii ni muhimu katika safari ya uponyaji. Elimu ni silaha
kubwa,” anasema na kuongeza,
“Utambuzi wa mapema unaokoa maisha, kila mmoja awe balozi wa elimu ya saratani ili kuokoa maisha ya wengi zaidi,” anasisitiza Dkt Juma.
BALOZI NA TANZANIA
“Ongezeko
la muda wa kuishi [life expectancy] kwa watu wa Tanzania limechangia pia
kuongezeka kwa visa vya saratani,” anasema Balozi Charlotta.
Anaongeza
“Watu wanaishi muda mrefu zaidi, na kadri miaka inavyoongezeka [kwa mujibu wa
shahidi za ki-sayansi], ndivyo uwezekano wa kupata saratani unavyoongezeka.
“Hivyo
Watanzania wanahitaji kujifunza zaidi kuhusu namna ya kuishi kwa afya bora lishe,
mazoezi pamoja na kuzingatia uchunguzi wa mapema,” anashauri.
Anasisitiza
ni muhimu wanawake na wasichana vijana kufahamu miili yao, hasa kupitia
kuchunguza binafsi matiti yao mara kwa mara.
“Pia
kwena hospitalini, kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi kwa kipimo cha mammografia
kadri umri unavyoongezeka,” anashauri.
SWEDEN & TANZANIA
Kwa
upande wa ushirikiano wa kimataifa, anasema Serikali ya Sweden imekuwa bega kwa
bega na Tanzania kwa zaidi ya miaka 60 katika kuboresha huduma za afya.
“Tulisaidia
sana wakati wa mapambano dhidi ya UKIMWI na tumeendelea kushirikiana katika
kuboresha huduma za msingi za afya,” anabainisha.
Balozi
Charlotta anaongeza “Sasa tunasaidia zaidi katika kuelimisha jamii kupitia
matukio kama haya na kushirikiana na taasisi kama Shujaa Cancer Foundation pamoja
na Wizara ya Afya.
“Pia tunasaidia kampuni ya ki-Sweden inayotengeneza vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa saratani ya matiti (mammography), ili teknolojia hiyo ipatikane si tu mijini bali pia vijijini”.
TUVUNJE UNYANYAPAA
Pamoja
na hayo, anasisitiza elimu ni jambo la msingi kulizingatia kwa nguvu kubwa kwa
sababu ni ngao kubwa dhidi ya saratani.
“Tunahitaji
kuzungumza wazi wazi kuhusu saratani kama tunavyoongelea shinikizo la damu au
kisukari.
“Haitokani
na kurogwa na waganga wa kienyeji wala si laana. Hii ni changamoto ya hali ya
ki-afya ambayo inaweza kumpata mtu yeyote.
Anaongeza
“Miaka 100 iliyopita, 90% ya wanawake waliougua saratani ya matiti walifariki
dunia, lakini sasa hali imebadilika 90% wanatibiwa na kupona, wanaishi.







Chapisha Maoni